1.2 KiB
Taarifa ya Jumla:
Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.
Kwa mwanamuziki mkuu
"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"
Zaburi ya Daudi
Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.
Mbingu zinatangaza
Mbingu zinaelezwa kana kwamba ni mtu. "Mbingu zinaonesha" au "Mbingu zinaonekana kama zinatangaza"
anga zinafanya kazi yake ya mikono kujulikana
Anga zinaelezwa kana kwamba ni mwalimu. "anga zinaonekana kufanya kazi ya mikono ya Mungu kujulikana kwetu"
kazi yake ya mikono
"uumbaji wake" au "ulimwengu alioutengeneza"
maneno humwagika
Kilicho kizuri kuhusu uumbaji kinafananishwa na kuzungumza, kana kwamba uumbaji ni mtu. Kisha maneno hayo yanalinganishwa na maji wanayotiririka kila mahali. "Uumbaji ni kama mtu anayezungumza na kila mtu"
Hakuna mazungumzo au maneno ya kusemwa; sauti yao haisikiki
Misemo hii inaelza wazi kuwa mistari miwili ya kwanza ilikuwa sitiari. "Hakuna mazungumzo ya kweli wala maneo ya kusemwa; hakuna anyesikia sauti halisi kwa masikio yao"
sauti yao haisikiki
Tafsiri zingine zinasoma "ambapo sauti yao haisikiki," kusisitiza kuwa "mazungumzo" ya uumbaji yanapatikana kila sehemu.