forked from WA-Catalog/sw_tn
1018 B
1018 B
Maelezo ya Jumla
Katika 1:20-1:33 Hekima inaongelewa mithili ya mwanamke anayeongea na watu.
Hekima analia kwa sauti
"Hekima ni kama mwanamke ambaye hulia kwa sauti kuu"
hupaza sauti yake
Hii ni nahau "Huongea kwa sauti kuu"
katika viwanja
sehemu ambapo huweza kuwa na watu wengi. "kwenye soko" au "katika viunga vya mji"
kwenye kelele kuu za mitaa
sehemu ambapo mitaa yenye shughuli nyingi imeunganika au juu ya ukuta ambapo watu walioko kwenye kelele za mitaa wanaweza kuona na kusikia hekima ikiongea.
Hata lini, ninyi watu wajinga, mtapenda kuwa wajinga?
Hekima anatumia swali hili kuwakemea wasio na hekima. "Ninyi ambao ni wajinga lazima mkome kupenda kuwa wajinga"
wajinga
"bila uzoefu, isiyo komavu/uchanga"
Hata lini, ninyi wenye dhihaka, mtapenda dhihaka, na hata lini, ninyi wapumbavu, mtachukia maarifa?
Hekima anatumia swali hili kuwakema wenye dhihaka na wapumbavu. " Ninyi ambao hudhihaki lazima muache kupenda dhihaki, na ninyi wapumbavu lazima muache kuchukia maarifa"