1.4 KiB
Taarifa ya Jumla
Isaya anaendelea kuzungumza ujumbe wa Mungu kwa Shebna.
Itakuja kuwa katika siku hiyo
Hapa "siku" inawakilisha kipindi kwa ujumla. "'Itatokea katika kipindi hicho"
Eliakimu ... Hilkia
Haya ni majina ya wanamume.
Nitamvisha kwa gwanda lako na kumwekea juu yake mshipi wako
Yahwe kusababisha Eliakimu kuchukua nafasi ya Shebna katika kasri ya mfalme inazungumziwa kana kwamba Yahwe atamvisha Eliakimu katika nguo za Shebna ambazo zinawakilisha mamlaka yake katika kasri ya mfalme.
gwanda lako ... mshipi wako
Hapa gwanda na mshipi inawakilisha mamlaka katika kasri ya mfalme.
mshipi
Hii ni kipande cha nguo ambacho watu huvaa kuzunguka kiuno au kupita kifuani.
katika mkono wake
Hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala. "kwake"
Atakuwa baba
Eliakimu kutunza na kulinda watu wa Yuda inazungumziwa kana kwamba angekuwa baba yao. "Atakuwa kama baba"
katika nyumba ya Yuda
Hapa "nyumba" inawakilisha watu. "kwa watu wa Yuda"
Nitaweka ufunguo wa nyumba ya Daudi juu ya bega lake ... hakuna atakayefungua
Hapa "ufunguo" inawakilisha mamlaka. Hii inazungumzia Eliakimu kuwa na mamlaka ambayo hakuna mtu awezaye kumzuia kana kwamba alikuwa na ufunguo wa kasri na hakuna mtu mwingine awezaye kufunga au kufungua mlango. "Nitamweka kuwa msimamizi wa wale ambao hufanya kazi katika kasri ya mfalme, na anapofanya maamuzi hakuna atakayeweza kumpinga"