forked from WA-Catalog/sw_tn
903 B
903 B
Taarifa ya jumla:
Matukio ya sura hii yanatokea baadaya Nuhu kujenga safina, kukusanya chakula, na kukiweka ndani ya safina.
Njoo ...katika safina ...utakuja nao
"Ingia ... ndani ya safina .. chukua". Tafsiri nyingi husema "Nenda .. ndani ya safina .. chukua"
wewe
Neno hapa "wewe" linamaana ya Nuhu la lipo katika umoja.
nyumba yako
"familia yako"
mwenye haki mbele yangu
Hii inamaana ya kwamba Mungu alimwona Nuhu kuwa mwenye haki.
katika kizazi hiki
Hii inamaana ya watu wote ambao walikuwa wakiishi katika muda huo. "Kati ya watu wote wanaoishi sasa"
mnyama aliye safi
Huyu alikuwa ni myama ambaye Mungu aliruhusu watu wake wamle na kutoa sadaka.
wanyama wasio safi
Hawa ni wanyama ambao Mungu hakuruhusu watu wale au kutoa sadaka.
kuhifadhi kizazi chao
"ili kwamba waweze kuwa na kizazi kitakachoishi" au "ili kwamba, baada ya gharika, wanyama waendelee kuishi"