sw_tn/gen/04/06.md

1.1 KiB

kwa nini umekasirika na kwa nini uso wako umekunjamana?

Mungu alitumia maswali haya la balagha kumwambia Kaini ya kwamba hakuwa sahihi kuwa na hasira na kukunjamana sura. Yawezekana yalitumika kumpatia Kaini nafasi ya kutubu makosa yake.

Kama ... je hutapata kibali?

Mungu alitumia swali hili la balagha kumkumbusha Kaini juu ya jambo ambalo Kaini alipaswa kulifahamu. "Unajua ya kwamba ukifanya lilio sahihi, nitakukubali"

lakini kama hutafanya ... inakupasa uishinde

Mungu anazungumzia dhambi kana kwamba ni binadamu. "Lakini kama hutafanya kilicho sahihi, utatamani kufanya dhambi zaidi, na kisha utatenda matendo ya dhambi. Unatakiwa kukataa kuitii"

dhambi iko inakuotea ... kukutawala

Hapa dhambi inazungumziwa kama mnyama mwitu hatari anayesubiri nafasi ya kumshambulia Kaini. "utakuwa na hasira sana utashindwa kuizuia dhambi"

dhambi

Lugha ambazo hazina nomino yenye maana ya "dhambi" zaweza kutafsiri hii kama "tamaa yako kutenda dhambi" au "mambo mabaya unayotaka kufanya".

inakupasa uishinde

Yahwe anazungumzia tamaa ya Kaini kutenda dhambi kana kwamba ni mtu ambaye Kaini anapaswa kumtawala. "unapaswa kuitawala ili usitende dhambi"