sw_tn/act/21/intro.md

1.7 KiB

Matendo 21 Maelezo kwa Jumla

Muundo na Mpangilio

Matendo 21:1-19 Inaelezea safari ya Paulo kwenda Yerusalemu. Baada ya kuasili Yerusalemu,Waumini walimuambia kwamba Wayahudi walitaka kumdhuru .Walimwelezea pia alichopaswa kufanya ili wasimdhuru (Mistari 20-26). Ingawa Paulo alikifanya alichoambiwa na waumini,Wayahudi walijaribu kumuua. Warumi walimuokoa na wakampa nafasi ya kuwaongelesha Wayahudi.

stari wa Mwisho wa sura hii unaishia na sentensi isiyokamilifu kimaana. Tafsiri nyingi huwacha hiyo sentensi kama haijakamilika kama vile ULB hufanya.

Dhana maalum katika sura hii

"Wote wamejitahidi kuilinda sheria"

Wayahudi wa Yerusalemu walifuata sheria za Musa. Hata wale waliomfuata Yesu bado walizizingatia. Makundi yote yalifikiri kwamba Paulo alikuwa akiwaambia Wayahudi walio Uyunani wasifuate hizo sheria. Lakini watu wa Mataifa ndio Paulo alikuwa akiwahutubia.

Nadhiri za kuwafunga wanaume

Nadhiri ambazo Paulo na marafiki wake watatu walichukua ilikuwa ni kama ya Wanaume wa kujifunga kwa Nadhiri kwa vile walinyoa nywele zao (Matendo 21:32)

Watu wa Mataifa kwa hekalu

Wayahudi walimlaumu Paulo kwa kumleta mtu wa Mataifa katika sehemu maalum ya hekalu ambamo Mungu aliwaruhusu Wayahudi pekee kuingia. Wakafikiri kwamba Mungu alitaka wamuadhibu Paulo kwa kumuua. (Tazama: //en/tw/dict/bible/kt/holy)

Uraia wa Urumi

Warumi walidhani kwamba ni Warumi pekee yao waliostahili kuhudumiwa kwa haki. Wangewatenda watakavyo wale ambao hawakuwa raia wa Urumi lakini kwa Warumi waliwatendea kufuata sheria. Watu wamoja walizaliwa raia wa Roma na wengine wakaipa pesa serikali ya Warumi ili wawe raia.

<< | >>