sw_tn/act/13/32.md

1.3 KiB

Maelezo ya jumla

Nukuu ya pili hapa inatoka katika kitabu cha nabii Isaya.

Hivyo

Kiunganishi cha neno kinachoonyesha tukio kwamba tukio lililokwisha kupita ni kwasababu ya tukio lililokuwa limetangulia kutukia. Tukio la nyuma kabla ya lile lililofuata ni la kumfufua Yesu kutoka kwa wafu.

mababu zetu.

"mababu zetu" Paulo bado anaongea na Wayahudi na watu wa mataifa waliofuata desturi za Kiyahudi huko Antiokia Pisidia. Hawa walikuwa mababu wa kimwili wa Wayahudi na Mababu wa kiroho wa wakristo wa mataifa waliofuata desturi za Kiyahudi.

Mungu aliweka ahadi hizi

"Mungu amekwisha timiza hizo ahadi"

kwetu, watoto wao,

"Kwetu" inamaanisha wale watoto wa hao mababu"

katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai

"Kwa kumfanya Yesu kuwa mzima tena"

Hili pia liliandikwa katika Zaburi

kweli huu umeandikwa pia na Zaburi ya pili."

Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako

Hivi ni vyeo muhimu vinavyoeleza ule uhusiano kati ya Yesu na Mungu.

kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi

"Mungu alinena haya maneno juu ya kumfanya Yesu kuwa mzima tena ili asionekane na mauti tena"

Kutoka kwa wafu

"Wafu" ni neno linalowakilisha watu waliokwisha kufa. Atamfufua kutoka miongoni mwao na kumfanya kuwa mzima tena"

baraka halisi

"Baraka za kipekee"