sw_tn/act/13/06.md

1.4 KiB

Maelezo ya jumla

Mistari hii imetaja viwakilishi vingi vya majina kuelezea watu mbalimbali walio tajwa na mwandishi Luka.

katika kisiwa chote

Walitembelea kisiwa chote kutoka upande mmoja hadi upande mwingine wakiunena ujumbe wa Injili katika kila mji walimopita.

Pafo

Ni mji Mkuu wa kisiwa cha Kapro mahali Liwali alikuwa akiishi.

Walimkuta

Neno "Kumkuta" linamaanisha kuwa walimfikia bila ya kumtafuta.

Mtu fulani mchawi

"Mtu aliyekuwa akifanya kazu ya uchawi" au "Mtu aliyekuwa akifanya mambo yasiyo ya kawaida katika fani ya kimazingaombwe"

ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu

"Bar - Yesu" maana yake "Mwana wa Yesu". Hakukuwa na mahusiano yoyote ya karibu na Yesu Kristo". Jina Yesu lilikuwa ni jina la kawaida katkia wakati ule.

Mchawi huyu alishirikiana

"Alikuwa mara kwa mara pamoja na" au "Alikuwa mara kwa mara akiambatana na"

Liwali

Huyu alikuwa Kiongozi mtendaji Katika utawala mkoa wa dola ya Rumi.

aliyekuwa mtu mwenye akili

Hii ni historia ya maisha ya Liwali Sergio Paulus.

Lakini Elima "yule mchawi"

Huyu alikuwa Bar- Yesu, ambaly aliyekuwa akiitwa mchawi.

hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa

"Hivyo ndivyo jina lake katika lugha ya kigriki"

aliwapinga; alijaribu kumgeuza

"Aliwazuia akijaribu kumgeuza"

alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani

"Alijaribu kumshawishi Liwali kuiacha imani ya ujumbe wa Injli"