sw_tn/act/13/01.md

1.2 KiB

Sentensi unganishi

Luka anaanza kuzungumzia habari za safari za huduma ambazo kanisa la Antiokia liliwatuma Barnaba na Sauli.

Maelezo ya jumla

Mstari wa 1 unatupatia maelezo kuhusu watu wa kanisa la Antiokia.

Sasa katika kanisa la Antiokia,

"Kwa wakati, kanisa la Antiokoa"

Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaen

"Majina ya baadhi ya waliokuwepo katika kanisa la Antiokia

ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi

"Manaeni alikuwa pengine rafiki yake na Herode waliocheza michezo ya ujana pamoja naye"

kiongozi wa mkoa

"Mtawala wa sehemu au robo ya nchi"

Wakati

Neno hili linatambulisha matukio mawili yaliyokuwa yanatendeka kwa wakati mmoja.

Niteengeeni pembeni

"Nitengeeni hao kwa kunitumikia mimi"

kazi niliyo waitia.

Linamaanisha, Mungu amewachagua kufanya hazi hii.

na kuweka mikono yao juu ya watu hawa

"Wakaweka mikono juu ya manaume hao ambao Mungu alikuwa amejitengea kwa kazi yake. Tendo hili lilionyesha kwamba viongozi walikubali kuwa Roho Mtakatifu alikuwa amewaita Barnaba na Sauli kwa kuifanya kazi hii."

wakawaacha waende.

"Wakawaacha waende zao" au "Wakawatuma wanaume hao kutenda kazi ambayo Roho Mtakatifu alikuwa amewatuma kuitenda"