sw_tn/1ti/04/01.md

1.2 KiB

Kauli unganishi

Paulo anamwambia Timotheo kile ambacho Roho anasema kitatokea na anamtia moyo kwa kile ambacho anapaswa kufundisha.

nyakati zijazo

Inaweza kumaanisha 1) nyakati za baadaye kuliko nyakati za Paulo, "katika nyakati zinazokuja" au "wakati ujao" au 2) Katika wakati wa Paulo mwenyewe, "katika wakati wa kipindi hiki kabla ya wakati wa mwisho"

kuacha imani

"kuacha kuamini katika Yesu" au "kuondoka katika kile ambacho walikuwa wanakiamini"

kuwa makini kusikiliza

"kutoa kipaumbele" au "kwa sababu wanasikiliza kwa makini" au "wakati wakisikiliza"

roho zidanganyazo na mafundisho ya kipepo

"roho zinazowalaghai watu na mambo ambayo mapepo yanafundisha"

kwa uongo na unafiki

"yanayofundishwa na wanafiki ambao wanawaambia uongo"

dhamiri zao zitakuwa zimechomwa moto

Huu mfano ni wa mabwana ambao walikuwa wakiweka chuma cha moto katika ngozi za watumwa au wanyama kutengeneza kovu ambalo linaonesha umiliki. Yaweza kumaanisha 1) alama ya kuchomwa kama kitu cha kuleta utambulisho, "Wanafanya hivi hata kama wanajiona kwamba ni wanafiki," au 2) dhamiri zao zimetiwa ganzi, "kana kwamba wameweka chuma cha moto katika dhamiri zao kuzifanya kuwa na ganzi"