sw_tn/1ti/01/09.md

1.1 KiB

Na tunajua hiki

"Hiyo ni, sisi tunaelewa hiki" au "Kwasababu tunatambua hili" au "Sisi pia tunajua hili"

haikutengenezwa kwaajili ya mtu mwenye haki

"haikutolewa kwa mtu mwenye haki" au "haikuwekwa kwa mtu anaye tii" au "hakupewa mtu ambaye ni mwenye haki mbele za Mungu"

kwaajili ya wale wauao baba na mama zao

"wauaji wa baba zao na mama zao" au "wale ambao huwaumiza kimwili baba na mama zao"

watu wasio na maadili kingono

Huu ni mfumo wa neno la kiume kwaajili ya malaya wa kike. Kwenye maeneo mengine ilitumika kama sitiari kwa watu wasiowaaminifu kwa Mungu, lakini katika suala hili maana inaonekana kuhusisha mtu yeyote ambaye analala na mtu mwingine nje ya ndoa.

mashoga

"wanaume ambao wanalala na wanaume wengine."

wale ambao wanateka watu kwaajili ya utumwa

"wale ambao wanateka watu kuwauza kama watumwa" au "wale ambao wanachukua watu kuwauza kama watumwa"

injili ya utukufu wa Mungu wa baraka

"injili ya kuhusu utukufu ambao ni mali ya Mungu wa baraka" au "injili ya utukufu na Mungu mbarikiwa"

ambayo nimeaminiwa

"ambayo Mungu amenipa mimi na akanifanya kuwajibika kwayo"