sw_tn/1ti/01/01.md

1.1 KiB

Maelezo ya jumla

Katika kitabu hiki, neno "Yetu" linamaanisha Paulo na Timotheo.

Paulo

"Mimi, Paulo, nimeandika barua hii." Lugha yako inaweza kuwa na njia tofauti ya kumtambulisha mwandishi wa barua. Tumia njia iliyo sahihi kwenu.

kulingana na amri ya

"kwa amri ya" au "kwa mamlaka ya"

Mungu Mwokozi wetu

"Mungu ambaye alituokoa sisi"

Kristo Yesu tumaini letu

Hapa neno "tumaini letu" humaanisha mtu ambaye tunaweka tumaini letu kwake. "Kristo Yesu, ambaye ni tumaini letu" au "Kristo Yesu katika yeye tunaweka ujasiri wetu"

mtoto wa kweli katika imani

Paulo anaongea juu ya uhusiano wa karibu kati ya Timotheo na Paulo kama ule wa baba na mtoto. Paulo anamchukulia Timotheo kuwa ni mtoto wake kwa kuwa alimfundisha kuwa na imani katika Kristo. Mfano wa tafasiri: "ambaye ni sawa na mtoto kabisa kwangu"

Neema, rehema, na amani

"Basi neema, rehema, na amani iwe kwenu," au "Basi ninyi mpate wema, rehema, na amani"

Mungu Baba

"Mungu, ambaye ni Baba yetu" ni jina la muhimu la Mungu.

Kristo Yesu Bwana wetu

"Kristo Yesu, ambaye ni Bwana wetu"