sw_tn/zec/14/20.md

803 B

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa

yatakuwa kama mabakuri mbele ya madhabahu

"Itakuwa takatifu kama mabakuri yaliyotumika madhabahuni"

kila chungu katika Yerusalemu na Yuda kitatengwa kwa ajili ya Yahwe wa majeshi

Aina mbalimbali ya vyungu na vifaa vingine vilifanywa maalumu ili kutumika hekaluni kwa ajili ya kumwabudu Yahwe na kwa sadaka. Vilikuwa maalumu, havikutumika kwa jambo lingine lolote.

Hakutakuwa na wafanyabiashara tena katika nyumba ya Yahwe wa majeshi

Ilikuwa ni desturi kwa wafanyabiashara kuwauzia watu vitu walivyoviitaji kwa ajili ya ibada ya Yahwe hekaluni. Baadhi ya tafasiri zina "Wakanaani" badala, kwa maana nakala ya Kiebrania yaweza kuwa na maana mbili: "wafanyabiashara" na "Wakanaani."