sw_tn/zec/14/09.md

905 B

Maelezo ya Jumla:

Mistari hii inaelezea vita ya mwisho kwa mji wa Yerusalemu na jinsi Mungu atakavyouokoa.

kutakuwa na Yahwe, Mungu mmoja, na jina lake pekee

"kutakuwa na Mungu mmoja pekee, Yahwe, atakayeabudiwa"

Araba... Geba... Rimoni

Haya ni majina ya maeneo

Yerusalemu itaendelea kuwa juu

Hii inamaanisha mwinuko wa mji wa Yerusalemu, kama mita 760 juu ya usawa wa bahari.

Yeye

Yerusalemu na miji mingine imetajwa kwa kiwakilishi cha jina la kike(she)

ataishi mahali pake mwenyewe

"ataishi mahali amekuwa akiishi daima"

lango la Benjamini... lango la kwanza... Lango la pembeni

Haya ni majina mbalimbali ya malango katika ukuta wa Yerusalemu.

Mnara wa Hananeli

Hii inamaanisha sehemu yenye nguvu katika ulinzi wa mji ukutani. Pengine ulijengwa na mtu aliyeitwa Hananeli.

shinikizo la mfalme

Pengine inamaanisha mahali mvinyo wa familia ya kifalme ulipotengenezewa.