sw_tn/zec/08/18.md

1.2 KiB

Kisha neno la Yahwe wa majeshi likanijia mimi

"Mimi" inamrejerea Zakaria.

Mfungo wa mwezi wa nne

Wayaudi waliomboleza katika kipindi cha sehemu ya mwezi wa nne wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ulikuwa wakati Wababeli walipovunja ukuta wa Yerusalemu. Mwezi wa nne ni wakati wa mwishoni mwa Juni na mwanzoni mwa Julai katika kalenda ya sasa.

mwezi wa tano

Wayaudu walifunga wakati wa sehemu ya mwezi wa tano wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ndio wakati Wababeli walipoliaribu hekalu la Yerusalemu. Mwezi wa tano ni wakati wa sehemu ya mwisho wa Julai na mwanzoni mwa Agosti katika kalenda ya sasa.

mwezi wa saba

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu katika mwezi huu Wayaudi waliokuwa wamebaki Yerusalemu walikimbilia Misri baada ya kuuawa kwake Gedalia, ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua kuwa gavana juu ya Yuda. Mwezi wa saba ni wakati wa mwishoni mwa Septemba na mwanzoni mwa Oktoba katika kalenda ya sasa.

mwezi wa kumi

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa kumi katika kalenda ya Kiebrania kwa sababu huu ni wakati Wababeli walipoanza kuuhsusu Yerusalemu. Mwezi wa kumi ni mwishoni mwa Desemba na mwanzoni mwa Januari katika kalenda ya Magharibi.