sw_tn/zec/07/04.md

1.3 KiB

katika wa tano

"mwezi wa tano"

katika mwezi wa saba

Wayaudi waliomboleza wakati wa sehemu ya mwezi wa saba wa kalenda ya Kiebrania kwa sababu katika mwezi huu Wayaudi waliokuwa wamebaki Yerusalemu walikimbilia Misri baada ya kuuawa kwake Gedalia, ambaye mfalme wa Babeli alikuwa amemteua kuwa gavana juu ya Yuda. Mwezi wa saba ni wakati wa mwishoni mwa Septemba na mwanzoni mwa Oktoba katika kalenda ya sasa.

kwa miaka hii sabini

Watu wa Israeli walikuwa wamekuwa watumwa kwa miaka 70 huko Babeli.

mlipokula na kunywa

Kifungu hiki kinamaanisha walipokula na kunywa katika sherehe kuheshimu jinsi Yahwe alivyokuwa ameandaa kwa ajili yao.

Je ni kweli mlifunga kwa ajili yangu?

Swali linatumika kuwalaumu Waisraeli kwa kutomweshimu Yahwe walipofunga.

Je! hamkula na kunywa kwa ajili yenu wenywewe?

Swali linatumika kuwalaumu Waisraeli waliosherehekea sherehe kwa kutomweshimu Yahwe kwa sherehe zao.

Yahwe alisema kwa kinywa cha manabii wa zamani

Zakaria anarejerea manabii wa zamani kwa kurejerea sehemu ya mwili wao uliosema neno la Yahwe.

Haya hayakuwa maneno yaleyale... upande wa magharibi?

Swali hili laweza kuandikwa kama taarifa: "Haya yalikuwa maneno halisi yaleyale... upande wa magharibi."

Ilikaliwa

"waliishi ndani yake"

chini ya vilima

Hivi ni vilima kabla haujafika kwenye milima.