sw_tn/rev/21/05.md

973 B

maneno haya ni ya hakika na kweli

Hapa "maneno" yanamaanisha ujumbe uliyounda. "ujumbe huu ni wakuaminika na wa kweli"

Alfa na Omega, mwanzo na mwisho

Misemo hii miwili inamaanisha jambo moja na inasisitiza asili ya milele ya Mungu .

Alfa na Omega

Hizi ni herufi za kwanza na mwisho katika alfabeti ya Kigriki. Maana zinazowezekana ni 1) "yule aliyeanzisha vitu vyote na anayevileta mwisho vitu vyote" au 2)"yule ambaye alikuwepo na ataendelea kuwepo". Kama haieleweki kwa wasomaji unaweza kufikiria kutumia herufi katika alfabeti zako. "Yeye ni A na Z" au "mwanzo na mwisho"

mwanzo na mwisho

Maana zinazowezekana ni 1)"yule aliyeanzisha vitu vyote na ambaye atasababisha vyote kufika mwisho" (UDB) au 2) "yule aliyekuwepo kabla ya vitu vyote na atakuwepo baada ya vitu vyote."

Kwa yeyote aonaye kiu ... maji ya uzima

Mungu anazungumzia hamu ya uzima wa mile kama vile ni kiu na mtu anayepokea uzima wa milele ni kama vile anakunywa maji yaletayo uzima.