sw_tn/rev/17/16.md

855 B

watamfanya kuwa mpweke na uchi

"kuiba kila kitu alichonacho na kumuacha bila kitu"

watamla mwili wake

Kumuangamiza kabisa inazungumziwa kama kula mwili wake. "watamuangamiza kikamilifu"

Maana Mungu ameweka mioyoni mwao kubeba kusudi lake kwa makubaliano ... yatakapotimia

Watakubali kumpa mnyama nguvu zao, lakini haitakuwa kwamba wanataka kumtii Mungu. "Kwa kuwa Mungu ataweka mioyoni mwao kukubali kumpa mnyama uwezo wao kutawala hadi maneno ya Mungu yatimie, na kwa kufanya hivi, watakamilisha mpango wa Mungu.

Mungu ameweka mioyoni mwao

Moyo unaashiria hamu. Kuwafanya kutaka kufanya kitu inazungumziwa kama kuweka mioyoni mwao. "Mungu amewafanya watake"

nguvu za kutawala

"mamlaka" au "mamlaka ya kifalme"

mpaka maneno ya Mungu yatakapotimia

Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "mpaka Mungu atimize alichosema kitatokea"