sw_tn/rev/16/04.md

925 B

akamwaga bakuli lake

Neno "bakuli" linamaanisha kile kilichomo. "kumwagwa divai kutoka katika bakuli lake" au " kumwaga ghadhabu ya Mungu kutoka katika bakuli lake"

mito na katika chemichemi za maji

Hii inamaanisha mikusanyiko yote ya maji safi.

malaika wa maji

Maana zinazowezekana ni 1) hii inamaanisha malaika wa tatu aliye juu ya kumwaga ghadhabu ya Mungu katika mito na chemichemi za maji au 2) huyu alikuwa ni malaika mwingine aliyekuwa juu ya maji yote.

Wewe ni mtakatifu

"Wewe" inamaanisha ni Mungu.

Wewe uliyepo na uliyekuwepo

"Mungu aliyepo na aliyekuwepo."

walimwaga damu za waamini na manabii

Hapa "walimwaga damu" inamaanisha kuuawa. "watu waovu waliwaua waamini na manabii"

umewapa wao kunywa damu

Mungu atawafanya watu waovu wanywe maji atakayoyabadili kuwa damu.

Nikasikia madhabahu ikijibu

Neno "madhabahu" hapa inamaanisha mtu madhabahuni. "Nikasikia mtu madhabahuni akijibu"