sw_tn/rev/13/11.md

634 B

Kauli Unganishi:

Yohana anaanza kuelezea mnyama mwingine anayetokeza kwenye maono yake.

akazungumza kama joka

Maneno makali yanazungumziwa kana kwamba ni muungurumo wa joka. "akazungumza kwa ukali kama joka azungumzavyo"

joka

Hili lilikuwa tambaazi kubwa kali, kama mjusi. Kwa wayahudi ilikuwa ni alama ya uovu na machafuko. Joka pia linatambulika katika mstari wa 9 kama "ibilisi au Shetani"

dunia na wale walioishi wakimuabudu

"watu wote duniani"

yule ambaye jeraha lake baya limepona

"yule aliyekuwa na jeraha baya lililopona"

jeraha baya

"jeraha baya." Hili ni jeraha kubwa linaloweza kusababisha mtu kufa.