sw_tn/rev/11/03.md

1002 B

Kauli Unganishi:

Mungu anaendelea kuzungumza na Yohana.

wamevaa magunia

"wamevaa nguo chafu za maombolezo" au "watavaa nguo zilizokwaruzwa kuonesha kuwa walikuwa na masikito sana"

Hawa mashahidi ni

Yohana anaelezea hawa mashahidi ni kina nani.

Hawa mashahidi ni miti miwili ya mizeituni na vinara viwili

"Hawa mashahidi wawili ndio waliowakilishwa na miti miwili ya mizeituni na vinara viwili"

miti miwili ya mizeituni na vinara viwili

Yohana anategemea wasomaji wake wajue kuvihusu kwa sababu nabii mwingine aliandika kuvihusu miaka mingi kabla. "miti miwili ya mizeituni na vinara viwili vinavyosemwa na maandiko"

moto hutoka vinywani mwao na kuwadhuru adui zao

Kwa sababu hii inahusu matukio ya mbeleni, inaweza kuwekwa katika wakati ujao.."moto utatoka vinywani mwao na kuwateketeza adui zao"

moto ... kuwadhuru adui zao

Moto kuwaka na kuua watu inazungumziwa kana kwamba mnyama anayeweza kuwala. "moto .. utawateketeza adui zao" au "moyo ... utawachoma kabisa adui zao"