sw_tn/rev/07/01.md

804 B

Taarifa ya Jumla:

Yohana anaanza kueleza maono ya watumishi 144,000 wa Mungu waliotiwa muhuri. Hii inatendeka katikakati ya pale ambapo Mwanakondoo anafungua muhuri wa sita na muhuri wa saba.

kona nne za dunia

Dunia inazungumziwa kama vile ni tambarare na mraba kama kartasi. Usemi "kona nne" humaanisha kaskazini, kusini, mashariki na magharibi.

muhuri wa Mungu aliye hai

Neno "muhuri" hapa humaanisha kifaa kinachotumika kuweka alama katika muhuri wa nta. Na hapa, hiki kifaa kitatumika kuweka alama katika watu wa Mungu. "alama" au "stampu"

tumekwishaweka muhuri katika paji za vichwa

Neno "muhuri" hapa linamaanisha alama. Hii alama inaonesha kwamba hawa ni watu wa Mungu na atawalinda. "weka alama katika paji za vichwa"

paji za vichwa

Paji la kichwa ni juu ya uso, juu ya macho.