sw_tn/rev/03/17.md

797 B

wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi

Yesu anazungumzia hali yao ya kiroho kama vile anazungumzia hali yao ya kimwili. "Nyie ni kama watu duni sana, wakusikitisha, maskini, vipofu, na uchi."

Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto

Dhahabu iliyo safishwa katika moto ni safi na ya dhamani sana. Hapa wokovu ambao Yesu anawapa binadamu unazungumziwa kama dhahabu. "Pokeeni kutoka kwangu kilicho cha dhamani zaidi kama vile ni dhahabu iliyotakaswa katika moto."

upate kuwa tajiri

Hii humaanisha utajiri wa kiroho, kuishi maisha yenye dhamani sana mbele za Mungu. "wawe matajiri kiroho" au "aishi maisha ya dhamani zaidi"

nguo nyeupe za kumetameta

Nguo nyeupe zinaonesha utakatifu. "utakatifu kama nguo nyeupe"

upate kuona

Kuona inamaanisha kuelewa ukweli.