sw_tn/psa/147/015.md

408 B

amri yake inakimbia haraka sana

Mwandishi anaelezea amri za Mungu kana kwamba ni mjumbe anayekimbia haraka kufikisha ujumbe wa Mungu.

Huifanya theluji kama sufu, husambaza jalidi kama majivu

Hii inasisitiza jinsi ilivyo rahisi kwake kufanya hivi vitu. Hufunika ardhi kwa theluji kwa urahisi kama mtu anavyofunika kitu kwa blangeti wa sufu. Na huondoa jalidi kwa wepesi kama upepo unavyopuliza majivu.