sw_tn/psa/144/007.md

768 B

Nyosha mkono wako toka juu; niokoe na maji mengi

Daudi anazungumza kana kwamba Mungu alikuwa kwenye ardhi juu ya mafuriko na ana mikono ya kimwili ambayo angeweza kumvuta Daudi kutoka kwenye mafuriko. Mafuriko ni sitiari ya taabu zilizosababishwa na "wageni." "Unaweza kutenda, nisaidie nizishinde taabu zangu"

kutoka mkono wa wageni

Hapa "mkono" unaashiria nguvu."kutoka katika nguvu ya wageni"

Midomo yao inazungumza uongo

"Wanazungumza uongo"

mkono wao wa kuume ni uongo

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi anazungumzia utamaduni wa kuinua mkono wa kuume ili kuapa kuwa anachotaka kusema mtu mahakamani ni kweli, "wanadanganya hata wanapoapa kusema ukweli," au 2) "mkono wa kuume" ni sitiari ya nguvu, "kila kitu walichopata, wamepata kwa kusema uongo"