sw_tn/psa/144/001.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

mwamba wangu

Maana zinazowezekana ni1) "yule ambaye ananiweka salama" au 2) "yule anayenipa nguvu"

anayefunza mikono yangu kwa ajili ya vita na vidole vyangu kwa mapambano

Maneno "mikono" na "vidole" zinamaana ya "mimi." "anayeniandaa kwa ajili ya vita" au ""anayeniandaa kwa ajili ya mapambano"

uaminifu wangu wa agano

"yule ambaye ananionesha uaminifu wa agano"

ngome yangu ... namkimbilia

Mwandishi wa zaburi anatumia sitiari kusisitiza kwamba Yahwe atamlinda.

mnara wangu wa juu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngome inayomlinda dhidi ya mashambulizi. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi na hatari.

ngao yangu

Daudi anamzungumzia Yahwe kana kwamba ni ngao inayomlinda askari. Yahwe ndiye anayemlinda Daudi dhidi ya hatari.

yule ambaye namkimbilia

Kwenda kwa Yahwe kunazungumziwa kama kumkimbilia. "yule ambaye ninaenda kwake kwa ajili ya ulinzi"

yule unayedhibiti mataifa chini yangu

"yule anayenisaidia kuyashinda mataifa mengine"