1.2 KiB
anipige
Mwandishi anazungumza kana kwamba kukemewa ni kumpiga mtu kimwili. "nikemee" au "nipige ili nisikie anaponirekebisha"
itakuwa kama fadhili kwangu
"anaponipiga, nitajua kuwa yule anayenipiga ananitendea fadhila"
itakuwa kama mafuta kichwani kwangu
Maana zinazowezekana ni kwamba mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba mtu anayemsahihisha anamwekea mafuta kichwani mwake 1) kumpa heshima. "anaponisahihisha, nitajua kuwa yule anayenisahihisha ananitendea jambo jema" au 2) kufanya kichwa chake kipate unafuu.
na kichwa changu kisikatae kukubali
Kichwa kinamwakilisha mtu. "na niikubali kwa furaha"
maombi yangu daima ni dhidi ya matendo yao ya uovu
Maneno "matendo ya uovu" ni njia nyingine ya kusema watu waliotenda hayo matendo maovu. "Huwa naomba kwamba Yahwe awazuie watu waovu kutenda mambo maovu"
Viongozi wao watatupwa chini
Maana zinazowezekana ni 1) "Mtu atawatupa viongozi wao chini" au 2) "Viongozi wao watawatupa chini."
genge
ardhi yenye mteremko wa ghafla
mifupa yetu imetawanywa
Maana zinazowezekana ni 1) "watu wametupa mifupa yetu pande tofauti" au 2) kama matokeo ya kuanguka katika genge. "miili yetu imevunjika na mifupa yetu imelala ovyo.