forked from WA-Catalog/sw_tn
936 B
936 B
Taarifa ya Jumla:
Katika mistari hii miwili mwandishi anafananisha adui wa Israeli na mafuriko ya maji.
Maji yangetubeba ... yangetuzamisha
Hii inaendela kauli ya nadharia tete kutoka mstari uliopita. Inaeleza matokeo ambayo hayakutokea, kwa sababu Yahwe alikuwa upande wao. "Maji hayakutubeba ... hayakutuzamisha"
Maji ... mbubujiko wa nguvu ... maji ya nguvu
Misemo hii ina maana sawa.
yangetubeba ... ungetulemea ... yangetuzamisha
Misemo hii ina maana sawa.
Maji yangetubeba
Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya mji. "Adui zetu wangetushinda kwa urahisi"
mbubujiko wa nguvu ungetulemea
Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya maji ambayo yangewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetulemea"
maji ya nguvu yangetuzamisha
Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mto wenye hasira kali ambao ungewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetuangamiza"