sw_tn/psa/124/004.md

936 B

Taarifa ya Jumla:

Katika mistari hii miwili mwandishi anafananisha adui wa Israeli na mafuriko ya maji.

Maji yangetubeba ... yangetuzamisha

Hii inaendela kauli ya nadharia tete kutoka mstari uliopita. Inaeleza matokeo ambayo hayakutokea, kwa sababu Yahwe alikuwa upande wao. "Maji hayakutubeba ... hayakutuzamisha"

Maji ... mbubujiko wa nguvu ... maji ya nguvu

Misemo hii ina maana sawa.

yangetubeba ... ungetulemea ... yangetuzamisha

Misemo hii ina maana sawa.

Maji yangetubeba

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya mji. "Adui zetu wangetushinda kwa urahisi"

mbubujiko wa nguvu ungetulemea

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mafuriko ya maji ambayo yangewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetulemea"

maji ya nguvu yangetuzamisha

Hapa adui wa Mwandishi wanazungumziwa kana kwamba ni mto wenye hasira kali ambao ungewazamisha Waisraeli. "adui zetu wangetuangamiza"