sw_tn/psa/120/003.md

870 B

Atakuadhibuje, na nini zaidi atafanya kwako, wewe mwenye ulimi wa udanganyifu?

Mwandishi anauliza swali hili kama mwongozo wa kueleza kitu ambacho Mungu atafanya kwa waongo. Swali linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hivi ndivyo Mungu atakavyo kuadhibu, hiki ndicho atakachofanya kwako, wewe mwenye ulimi wa udanganyifu."

wewe mwenye ulimi wa udanganyifu

Hapa "ulimi wa udanganyifu" inamwakilisha mtu anayezungumza uongo. "wewe unayesema uongo"

Atakuadhibu kwa mishale ya shujaa

Mwandishi anazungumzia Mungu kuwaadhibu kwa ukali waongo kana kwamba Mungu anawapiga kwa mishale. "Atakuadhibu kwa ukali, kana kwamba anawapiga kwa mishale ya shujaa"

iliyochongwa juu ya makaa ya moto ya mti wa mfagio

Hii inamaansiha jinsi watu walivyounda ncha ya mshale katika moto. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "aliyochonga juu makaa ya moto ya mti wa mfagio"