sw_tn/psa/118/005.md

761 B

akaniweka huru

Mwandishi anazungumzia Yahwe kumwokoa kutoka kwenye huzuni kana kwamba Yahwe alimtoa kutoka sehemu ya kifungo hadi sehemu pana ya wazi ambapo angeweza kusogea kwa uhuru.

mtu atanifanya nini?

Mwandishi anauliza swali hili balagha kusisitiza kuwa hakuna kitu ambacho mtu anaweza kufanya kumuumiza kwa kuwa Yahwe yuko pamoja naye. "watu hawawezi kufanya chochote kunidhuru"

Yahwe yuko upande wangu kama msaidizi wangu

Kuwa upande wa mtu ni lahaja inayoashiria kuwa mtu anakubaliana na atamsaidia mtu mwingine. "Yahwe ananikubali na atanisaidia"

nitatazama kwa ushindi juu ya wale wanaonichukia

Inadokezwa kuwa Yahwe ndiye atakayewashinda adui wa mwandishi, wakati mwandishi akitazama. "Nitamwona Yahwe akiwashinde wote wanaonichukia"