sw_tn/psa/114/005.md

1017 B

Taarifa ya Jumla:

Mistari ya 5-6 ina maswali manne ya balagha. Jibu linalotarajiwa kwa kila swali linapatikana katika mstari wa 7, "kwa sababu ya uwepo wa Bwana."

uliruka kama kondoo dume ...uliruka kama wanakondoo

Mwandishi anazungumzia milima na vilima kana kwamba zilikuwa hai. Inawezekana anazungumzia tetemeko anapoelezea uoga wao kwenye uwepo wa Yahwe jinsi wanavyoruka kama kondoo dume na wanakondoo. "Ilikuwa kana kwamba milima ilitikisika kama kondoo dume wanaoruka na vilima vilitikisika kana kwamba wanakondoo wanavyoruka.

Tetemeka dunia, mbele ya Bwana, kwenye uwepo wa Mungu wa Yakobo

Misemo miwili ya mwisho ina usambamba. Kitenzi kinaweza kuwekwa kwenye mstari wa pili. "Tetemeka dunia, mbele ya Bwana, tetemeka mbele ya uwepo wa Mungu wa Yakobo"

Tetemeka dunia

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi anazungumzia dunia kana kwamba ni mtu na anaiamuru kutetemeka kwa uoga mbele za Mungu au 2) neno "dunia" ni njia nyingine ya kusema wale wanaoishi duniani. "Tetemekeni, watu wote duniani"