sw_tn/psa/114/003.md

795 B

Bahari lilitazama na kutoroka

Mwandishi anazungumzia bahari la Matete kana kwamba lilikuwa ni mtu aliyetoroka wakati Yahwe akiwaongoza watu wa Israeli kupita nchi kavu. "Ni kana kwamba bahari lilitazama na kutoroka"

Yordani ikageuka

Mwandishi anazungumzia mto Yordani kana kwamba ni mtu aliyerudi nyuma wakati Yahwe akiwaongoza watu wa Israeli kwenye nchi kavu. "ilikuwa kana kwamba Yordani ilirudi"

Milima ikaruka kama kondoo dume, vilima vikaruka kama wanakondoo

Mwandishi anazungumzia milima na vilima kana kwamba zilikuwa hai. Inawezekana anazungumzia tetemeko anapoelezea uoga wao kwenye uwepo wa Yahwe jinsi wanavyoruka kama kondoo dume na wanakondoo. "Ilikuwa kana kwamba milima ilitikisika kama kondoo dume wanaoruka na vilima vilitikisika kana kwamba wanakondoo wanavyoruka.