sw_tn/psa/110/002.md

1.0 KiB

Taarifa ya jumla:

Daudi anaendelea kuzungumza na mfalme

Yahwe ataishikilia fimbo ya nguvu yako

Hapa Daudi anamzungumzia Yahwe kupanua eneo analotawala mfalme kama kushikilia fimbo yake. "Yahwe atapanua eneo ambalo unatawala kwa uwezo"

tawala juu ya adui zako

"Mfalme, tawala kati ya adui zako." Hii inasemwa kwa mfalme kama amri.

kwa hiari yao wanyewe

"kwa uamuzi wao." Hii inamaanisha watachagua kumfuata mfalme.

katika siku ya uwezo wako

Hii inamaanisha siku ambayo mfalme atawaongoza watu wake vitani. Hii inaweza kuelezwa wazi. "katika siku utakapoliongoza jeshi lako vitani"

kutoka tumbo la alfajiri ... kama umande

Daudi anaelezea umande kama mtoto ambaye anazaliwa na umande. "asubuhi ... kama umande"

kutoka tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande

Daudi anamwambia mfalme kuwa atakuwa na nguvu za ujana kila asubuhi kwa kumfananisha na jinsi umande unavyotokeza mapema kila asubuhi. "kila asubuhi utajazwa na nguvu za ujana kukuhimili kama kila asubuhi umande unavyotokea kumwagilia na kuhimili ardhi"