sw_tn/psa/105/037.md

845 B

Aliwaleta Waisraeli nje wakiwa na fedha na dhahabu

Waisraeli walipoondoka Misri walichukua fedha na dhahabu pamoja nao. "Aliwatoa Waisraeli kutoka Misri pamoja na fedha na dhahabu katika milki yao"

hakuna wa kabila lake waliojikwaa njiani

Hakuna aliyebaki nyuma. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya chanya. "makabila yake yote yaliweza kufanya safari hiyo"

Misri ilifurahi

Hapa "Misri" ina maana ya watu ambao wanaishi Misri. Watu wa Misri alifurahi.

Alitandaza wingu kuwa mfuniko

Hapa mtunga zaburi anafafanua Yahwe kuweka wingu angani kana kwamba alikuwa akitandaza nje vazi. Wingu lilikuwa "linafunika" kuwalinda kutoka na jua. "Aliweka wingu angani kuwalinda kutoka na jua na joto"

kutengeneza moto kutoa mwanga usiku

Yahwe aliweka nguzo ya moto angani kutoa mwanga wakati wa usiku. "aliweka moto angani kutoa mwanga usiku"