sw_tn/psa/096/011.md

1.4 KiB

Acha mbingu zifurahi, na dunia ishangilie

Maana zinazowezekana ni 1) mwandishi wa zaburi anazungumza kana kwamba "mbingu" na "dunia" zina hisia kama watu. "Acha iwe kana kwamba mbingu zimefurahi na dunia kushangilia" au 2) "Acha wale wanaoishi mbinguni wafurahi na wale wanaoishi duniani washangilie"

acha bahari liungurume na kile kinacholijaza kipige kelele ya furaha

"acha sauti iwe kama watu wengi wanamsifu Yahwe, na acha iwe kana kwamba wale wanaoishi baharini na kupiga kelele kwa furaha"

Acha mashamba yashangilie na vyote vilivyomo

"Acha mashamba na vyote vilivyomo vishangilie." Mwandishi anazungumza kana kwamba "mashamba" na wanyama wanaoishi humo wana hisia kama watu. "Acha iwe kana kwamba mashamba yenyewe na wanyama wote wanaoishi humo washangilie"

Kisha acha miti yote msituni ipige kelele

"Kisha miti yote msituni zitapiga kelele"

Anakuja kuhukumu dunia. Atahukumu dunia ... na watu

Misemo hii mitatu ina maana za kufanana; misemo miwili ya mwisho inatumika kuimarisha ule wa kwanza.

kuhukumu ... atahukumu

Maana nyingine inayowezekana ni "kutawala ... atatawala"

Ataihukumu dunia kwa haki yake

Hapa "dunia" inamaanisha watu wa duniani. "Atawahukumu watu wote wa dunia kwa haki."

watu kwa uaminifu wake

"atawahukumu watu kwa uaminifu wake"

kwa uaminifu wake

Maana zinazowezekana ni 1) "kwa usawa, kulingana na kile anachojua kuwa kweli" au 2) "kutumia kigezo kile kile kwa watu wote."