sw_tn/psa/089/049.md

1.1 KiB

Bwana, yako wapi matendo yako ya kale ya uaminifu wako wa agano ulioahidi kwa Daudi katika ukweli wako?

Mwandishi anatumia swali kumwomba Bwana kuwa mwaminifu kwa agano lake na Daudi. "Bwana, kuwa mwaminifu kwa agano lako na Daudi kama ulivyokuwa kipindi cha nyuma"

Ita akilini

Mwandishi anamwomba Mungu kuleta hili katika kumbukumbu yake. "Kumbuka" au "Zingatia"

kejeli iliyolengwa kwa watumishi wako

Hapa "watumishi wako" inamaanisha watu wa Israeli. "jinsi wanavyotukejeli, watumishi wako"

jinsi ninavyobeba moyoni mwangu matusi mengi sana kutoka kwa mataifa

Hapa "moyo" unawakilisha hisia za mtu. "Ninavumilia matusi mengi sana kutoka kwa watu wa mataifa" au " Ninateseka kwa sababu watu wa mataifa wananitukana"

kutoka kwa mataifa

Hapa "mataifa" inawakilisha watu wa mataifa.

Adui zako wanatupa matusi

Adui kupiga kelele za matusi kwa mfalme inazungumziwa kana kwamba matusi ni kitu ambacho adui wanamtupia mfalme kwa nguvu.

wanakejeli hatua za watiwa mafuta wako

Hapa "hatua" inawakilisha pale ambapo mfalme anaenda. "wanamkejeli mtiwa mafuta wako popote aendapo"