sw_tn/psa/089/046.md

1.3 KiB

Hadi lini, Yahwe? Utajificha, milele?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kuwa hataki Mungu aendelee kumkataa mfalme. "Tafadhali, Yahwe, usikatae kumsaidia mfalme milele."

Utajificha

Mungu kutomsaidia mfalme inazungumziwa kana kwamba Mungu alikuwa anajificha kwake. "Je! Utakataa kumsaidia mfalme"

Hadi lini hasira yako itawaka kama moto?

Mwandishi anatumia swali kusisitiza kuwa hataki Mungu aendelee kubaki na hasira. "Tafadhali usiendelee kuwa na hasira"

hasira yako itawaka kama moto

Mungu kuwa na hasira sana inazungumziwa kana kwamba hasira yake ilikuwa moto mkali.

kwa ubatili gani umewaumba watoto wote wa mwanadamu

"kwamba umewaumba watu wote kufa kibatili"

watoto wote wa mwanadamu

Hii inamaanisha wanadamu kwa ujumla. "wanadamu" au "watu"

Nani anaweza kuishi na asife, au kuokoa maisha yake mwenyewe kutoka katika mkono wa kuzimu?

Mwandishi anatumia maswali haya kusisitiza kuwa watu wote watakufa. "Hakuna mtu anayeweza kuishi milele au kujifufua baada ya kufa"

kuokoa maisha yake mwenyewe kutoka katika mkono wa kuzimu

Hapa "mkono" unamaanisha uwezo. Mwandishi anazungumzia kuzimu kana kwamba ni mtu aliye na nguvu juu ya wale waliokufa. Maana zinazowezekana ni 1) mtu hawezi kujifufua baada ya kufa au 2) mtu hawezi kujizuia kufa.