sw_tn/psa/082/001.md

944 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Zaburi ya Asafu

"Hii ni zaburi ambayo Asafu aliandika"

mkusanyiko mtakatifu

"baraza la mbinguni" au "mkutano wa mbinguni"

anapitisha hukumu

"anatoa hukumu." Nomino dhahania "hukumu" inaweza kuelezwa kama kitenzi. "anahukumu"

miungu

Maana zinazowezekana ni 1) hivi ni viumbe vingine vya kiroho vinavyoishi mbinguni. "viumbe vitakatifu" au "mahakimu wa mbinguni" au 2) hawa ni mahakimu binadamu ambao Mungu amewachagua. Vyovyote vile, haimaanishi ni miungu kama Yahwe alivyo Mungu. Inamaanisha Mungu amewapa uwezo mkubwa na mamlaka. "watawala"

Hadi lini utahukumu bila haki na kuonesha upendeleo kwa waovu?

Yahwe anatumia swali kukemea miungu kwa kutowahukumu watu kwa haki.

Sela

Hili linaweza kuwa neno la kimuziki linalowaongoza watu jinsi ya kuimba au kujecheza vyombo hapa. Tafsiri zingine huandika neno hili la Kiebrania, na zingine haziliweki.