sw_tn/psa/080/009.md

983 B

Taarifa ya Jumla:

Asafu anazungumza kwa niaba ya Israeli. Anaanza katika mstari wa 8 kuzungumzia jinsi Mungu alivyowaweka Israeli katika nchi yao kana kwamba Mungu alikuwa ni mtu anayesafisha ardhi ili kupanda mzabibu.

Ulisafisha nchi kwa ajili yake

"Ulisafisha nchi kwa ajili ya mzabibu"

ikasika mzizi

""mzabibu ulikamata mzizi" au "mzabibu ulianza kuota"

kuijaza nchi

"matawi yake yakafunika nchi"

Milima ilifunikw kwa kivuli chake, seda za Mungu kwa matawi yake

"kivuli chake kilifunika milima, matawi yake seda za Mungu"

seda za Mungu kwa matawi yake

"na seda za Mungu zilifunikwa kwa matawi yake" "namatawi yake yalifunika seda za Mungu"

seda za Mungu

Maana zinazowezekana ni 1) "miti ya seda mirefu zaidi," miti ya seda iliyoota kwenye "milima" katika nchi ya Lebanoni kaskazini mwa Israeli, au 2) "Miti ya seda ya Mungu."

bahari

bahari ya Mediteranea magharibi mwa Israeli

vichipukizi

sehemu za mimea ambazo zinaanza kutokeza kutoka ardhini