sw_tn/psa/078/050.md

854 B

Taarifa ya Jumla:

Mwandishi anaendelea kuelezea kile ambacho Mungu alifanya kwa Wamisri.

Akasambaza njia kwa ajili ya hasira yake

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hasira yake kana kwamba ni mtu anayeweza kumtazama Yahwe akijiandaa kuwaadhibu watu kana kwamba alikuwa akitengeneza barabara kwa ajili ya mtu kutembelea. "Alikuwa na hasira sana hadi alifanya yote awezayo kuwadhuru" au "Ilikuwa kana kwamba hasira yake ni jeshi na akalitengenezea barabara kwa ajili ya kutembelea"

hakuwaepusha na mauti

"hakuwaepusha Wamisri na kifo" au "hakuwaruhusu Wamisri kuishi"

aliwapa kwa mapigo

Asafu anazungumzia pigo kana kwamba ni mtu amabye alikuwa anaenda kuwadhuru Wamisri. "aliwafanya wote kuugua sana kwa pigo"

mzaliwa wa kwanza wa nguvu yao

"wanaume wao wa muhimu na bora zaidi"

katika mahema ya Hamu

"miongoni mwa familia za Misiri"