sw_tn/psa/074/012.md

1004 B

Taarifa ya Jumla:

Hii inaanzisha wazo jipya: Asafu anatangaza ukuu wa matendo ya Mungu katika historia ya watu.

Mungu amekuwa mwema tangu nyakati za zamani

Maana zinazowezekana ni 1) Asafu anazungumza kama mwakilishi wa Israeli, "Mungu amekuwa mfalme wetu tangu Israeli lilipokuwa taifa" au 2) "Mungu, mfalme wangu, alikuwa hai hata katika nyakati za kale."

akileta wokovu

"kuokoa watu"

Uliligawa ... ndani ya maji

Asafu inawezekana anazungumzia wakati ambao Mungu aliitoa Israeli kutoka Misri, akagawa bahari, akawaongoza Waisraeli kwenye nchi kavu, kisha kuzamisha jeshi la Farao.

Uliligawa bahara kwa nguvu yako

Asafu anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. "Una nguvu sana uliweza kufanya nchi kavu katikati ya bahari.

bahari

"maji makuu"

uliponda vichwa vya wanyama wakubwa ndani ya maji

Inawezekana Asafu anamzungumzia Farao na jeshi lake kama vile walikuwa wanyama wa baharini. "Ulipoua jeshi la Farao, ilikuwa kama umeponda vichwa vya wanyama wakubwa ndani ya maji"