sw_tn/psa/074/009.md

1.2 KiB

Taarifa ya jumla:

Asafu anamueleza Mungu kuhusu uharibifu anaouona.

Hatuoni ishara zingine tena

Maanza zinazowezekana ni 1) "Hatuoni tena ishara za miujiza kutoka kwa Mungu" au 2) "Alama zetu zote takatifu hazipo" au 3) kama kuzungumzia bendera na alama zajeshi, "Jeshi letu limeangamizwa kabisa."

Hadi lini, Mungu, adui atatupa matusi kwako?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Mungu, adui amekuwa akikurushia matusi kwa muda mrefu sana!"

Adui atakufuru jina lako milele?

Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Inaonekana kana kwamba hautamzuia adui kukufuru jina lako!"

atakufuru jina

Neno "jina" ni njia nyingine ya kusema Mungu mwenyewe. "anasema wewe ni mbaya" au "anakutukana"

Kwa nini unazuia mkono wako, mkono wako wa kuume?

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. Hii inaweza kutafsiriwa kama kauli. "Acha kuzuia mkono wako, mkono wako wa kuume!"

unazuia mkono wako

Hapa neno "mokono" ni njia nyingine ya kusema nguvu. "usionesha nguvu yako" au "usitumie nguvu yako kuwaangamiza adui zako"

mkono wako wa kuume

"mkono wako wenye nguvu zaidi"

Toa mkono wako wa kuume kutoka kwenye vazi lako

Mwandishi wa zaburi anamzungumzia Mungu kana kwamba ana mwili. "Acha kuficha nguvu yako na uchukue hatua"