sw_tn/psa/073/006.md

971 B

Taarifa ya Jumla:

Asafu anaendelea kueleza ambavyo wakati mwingine anataka kulalamika kwa Mungu kuhusu wale ambao wana "kiburi" na "waovu".

Kiburi kinawapamba kama mkufu shingoni; vurugu inawavika kama joho

Hii inamaanisha waovu wanawaonesha wote jinsi walivyo na kiburi na vurugu kana kwamba wamevaa mkufu au joho zuri.

mkufu ... joho

Hii inaonesha vitu ambavyo matajiri na watu muhimu huvaa.

mkufu

ni kama mnyororo mdogo uliotengenezwa na madini kama dhahabu ambayo huvaliwa shingoni.

Kutokana na upofu wa hivi huja dhambi

Kwa sababu ni kama watu vipofu ambao hawaoni waendako, wanatenda dhambi bila kujua. Kuwa kipofu ni njia nyingine ya kusema mtu hawezi kuona jinsi alivyo muovu.

mawazo maovu yanapitia mioyoni mwao

Hapa mwandishi wa zaburi anaelezea mawazo ya watu kana kwamba ni watu. Pia anaelezea uhalisia wa ndani wa watu waovu kana kwamba ni majengo ambao wanaweza kutembea humo. "ndani yao huwa wanawaza mambo mengine maovu ya kufanya"