sw_tn/psa/072/001.md

2.0 KiB

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Maana zinazowezekana kwa ajili ya kichwa cha habari "zaburi ya Sulemani" ni 1) Daudi aliandika zaburi hii kwa ajili ya Sulemani("mwana wa mfalme") au 2) Sulemani (ambaye, kama mwana wa Daudi, alikuwa "mwana wa mfalme") aliandika zaburi hii kama maombi juu yake mwenyewe au 3) mfalme mwingine aliandika kumhusu mwanaye kwa mtindo wa Sulemani. Watu kipindi hicho mara nyingi walijizungumzia kana kwamba walikuwa mtu mwingine. Ingawa, itakuwa vyema zaidi kutafsiri hii kana kwamba mwandishi wa zaburi anamzungumzia mtu mwingine na sio yeye mwenyewe.

Mpe mfalme amri zako za haki, Mungu, haki yako kwa mwana wa mfalme

Maana zinazowezekana ni 1) "Nipe mimi, mfalme, amri zako za haki, Mungu, haki yako kwa mwana wa mfalme" au 2) "Nipe mimi, mfalme, amri zako za haki, Mungu, haki yako kwangu, mwana wa mfalme." Watu kipindi hicho mara nyingi walijizungumzia kana kwamba walikuwa mtu mwingine. Ingawa, itakuwa vyema zaidi kutafsiri hii kana kwamba mwandishi wa zaburi anamzungumzia mtu mwingine na sio yeye mwenyewe.

Mpe mfalme amri zako za haki

"Mwezeshe mfalme kuhukumu kwa haki"

haki yako kwa mwana wa mfalme

"Mwana wa mfalme aweze kutenda yanayokupendeza wewe"

Ahukumu

Kama ni Daudi aliandika hii, anamzungumzia mwana wake, "mwana wa mfalme," anazungumzia wakati ambao mwana wake atakuwa mfalme. Kama ni Sulemani aliyeandika hii, hata kama anaandika kujihusu, itakuwa vyema kuandika kana kwamba anaandika kumhusu mtu mwingine. Vyovyote vile, "mfalme ahukumu" ndio tafsiri bora zaidi.

watu wako ... maskini wako

Mwandishi wa zaburi anazungumza na Mungu.

na maskini wako

"na mfalme awahukumu watu wako maskini"

Milima itoe amani ... na vilima vitoe haki

Mwandishi wa zaburi anazungumzia watu wa Israeli kana kwamba ni milima na vilima ambapo wanaishi. Anazungumzia milima na vilima kana kwamba ni nchi nzima ya Israeli, kana kwamba nchi ni bustani itoayo matunda, na amani na haki kana kwamba ndio matunda. "Watu wa wa nchini waishi kwa amabi ... wafanye kila kitu kwa haki"