sw_tn/psa/071/008.md

785 B

Mdomo wangu umejaa na sifa yako ... na heshima yako

Mwandishi wa zaburi anazungumzia hamu yake ya kumsifu na kumpa heshima Yahwe kwa maneno anayoyazungumza kana kwamba mdomo wake umejaa maneno kama unavyoweza kujaa chakula. "Mdomo wangu utajaa maneno yanayokusifu wewe ... yanayo kuheshimu wewe" au "Nitakusifu daima ... nitakupa heshima daima"

sifa yako

"maneno yanayo waambia watu jinsi ulivyo mkuu"

heshima yako

"maneno yanayo wasababisha watu wakupe heshima"

siku nzima

"wakati wote"

Usinitupe ... usiniache

Misemo hii miwili ina maana moja na inatumika kwa pamoja kwa ajili ya mkazo.

Usinitupe

"Usinilazimisheniende mbali na wewe." Kwa Mungu kumkataa inazungumziwa kana kwamba Mungu anamlazimisha kwenda mbali. "usinikatae"

usiniache

"usiniache milele"