sw_tn/psa/069/007.md

1.3 KiB

Kwa ajili yako

"Kwa niaba yako"

Nimebeba lawama

Lawama za adui wa mwandishi zinazungumziwa kana kwamba ni mzigo mzito ambapo alitakiwa kubeba. "Nimevumilia matusi ya adui zangu"

aibu imefunika uso wangu

Mwandishi anazungumzia aibu anayoihisi kana kwamba ni kitu kibaya usoni pake ambacho kila mtu anakiona vizuri. "Nimeaibika sana"

Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kana kwamba hakuwa sehemu ya familia yake mwenyewe. "Ndugu zangu hawanijui tena au kunikubali kabisa"

mgeni kwa ndugu zangu ... mgeni kwa watoto wa mama yangu

Misemo hii miwili inamaana moja. Inarudiwa kusisitiza mtengano na familia yake mwenyewe.

mgeni kwa watoto wa mama yangu

Mwandishi anajizungumzia mwenyewe kana kwamba hakuwa sehemu ya familia yake mwenyewe. "ndugu zangu hawanijui tena au kuniamini kabisa"

ari ya nyumba yako imenila

Mwandishi anazungumzia ari kwa ajili ya hekalu la Mungu kana kwamba ni mnyama pori unaommeza mwandishi. "ari niliyonayo kwa ajili ya nyumba yako inanimeza"

imenila

Lahaja hii inamaanisha ari ya mwandishi kwa ajili ya hekalu inateka mawazo na matendo yake yote. "inatawala kabisa kila kitu nachowaza na kufanya"

lawama ... zimeniangukia

Mwandishi anazungumzia lawama za adui wa Mungu kana kwamaba ni mawe yaliyopondwa kwa mwandishi. "wale wanaokulaumu piwa wanatuma lawama zao kwangu"