sw_tn/psa/068/019.md

788 B

hubeba mizigo yetu kila siku

"hubeba mizigo yetu mizito kila siku." Kujali kwa Bwana kwa ajili ya watu wake inazungumziwa kana kwamba alikuwa akibeba kwa uhalisia matatizo yao kama mzigo.

Mungu ambaye ni wokovu wetu ... Mungu wetu ni Mungu anayeokoa

Misemo inamaanisha kitu kimoja. "Mungu anayetuokoa ... Mungu wetu ni Mungu anayeokoa"

atapiga katika vichwa vya adui zake

Mungu anazungumziwa kana kwamba ni shujaa ambaye ataua adui zake kwa kuwapiga vichwani ili kuwaua. "atawaua adui zake kwa kuwapiga kichwani"

ngozi ya kichwa na nywele nyingi

Inaonekana kuwa utamaduni wa wanajeshi kutonyoa nywele zao wakati wa vita. "mafuvu yenye nywele ndefu"

wanaotembea katika makosa dhidi yake

Kumkosea Mungu inazungumziwa kama kutembea kwenye makosa. "kumkosea mara kwa mara"