sw_tn/psa/068/011.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla:

Daudi anaendelea hadithi ya safari ya Waisraeli katika jangwa. Katika sehemu hii ya hadithi, Waisraeli wanashinda vitani dhidi ya adui zao.

wale walioyatangaza ... jeshi kubwa

Idadi kubwa ya watu walisema ujumbe wa Bwana kwa wengine. Wanazungumziwa kana kwamba ni jeshi kubwa. Kwa kuwa msemo huu ni wa kike, tafsiri zingine hutafsiri hii kama, "wanawake walioyatangaza ... jeshi kubwa."

Wafalme wa majeshi ... kwa nini mlifanya hivi?

Taarifa hii katika 68:11 imepangwa vingine ili maana yake ieleweke kwa wepesi zaidi.

Wafalme wa majeshi wanatoroka, wanatoroka

Wafalme wanawakilisha majeshi kamili. Inaeleweka kuwa wanatoroka kwa sababu wameshindwa na jeshi la Israeli. "Wafalme na majeshi yao wanatutoroka kwa sababu wameshindwa"

nyara

mali vinavyochukuliwa kutoka kwa jeshi lililoshinwa na kuletwa kwa maskani ya jeshi lililo shinda.

njiwa waliofunikwa kwa fedha ... dhahabu

Hii inamaanisha kuwa baadhi ya vitu vilivyotekwa nyara ni vya thamani sana kwa sabau vimefunikwa kwa mawe ya thamani.

Wakati baadhi ya nyie watu mlipobaki katika zizizi za kondoo, kwa nini mlifanya hivi?

Swali hili linatumika kukemea watu ambao hawakushiriki vitani. "Wale waliobaki katika zizi za kondoo wasinge baki; wangeenda vitana."