sw_tn/psa/066/010.md

859 B

Umetuleta kwenye wavu

Mwandishi anazungumzia adhabu ya Mungu kana kwamba Mungu aliwashika watu wake katika wavu.

wavu

mtego kwa ajili ya ndege au mnyama

umeweka mzigo mkubwa viunoni mwetu

Mwandishi anazungumzia kile ambacho watu wamestahamili kama kulazimika kubeba mizigo mizito migongoni mwao.

Umewafanya watu kuendesha juu ya vichwa vyetu

Hii ni picha ya kushindwa vibaya vitani. "Ni kana kwamba adui zetu wametushinda vitani na wameendesha vibandawazi vyetu juu ya miili yetu iliyoanguka"

tulipita katika moto na maji

Mungu aliwajaribu kwa maafa ya asili kama moto na mafuriko. "tuliteseka kama watu wanavyoteseka kutokana na moto na mafuriko"

sehemu yenye nafasi

Mwandishi anazungumzia baraka walizonazo sasa watu wa Israeli kana kwamba wameletwa katika nafasi kubwa ya wazi ambapo wako salama. "nafasi ya wazi ambapo tuko salama"