sw_tn/psa/062/001.md

899 B

Taarifa ya Jumla:

Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania.

Taarifa ya Jumla:

Zaburi hii ni wimbo kuhusu uaminifu wa Mungu.

Kwa mwanamuziki mkuu

"Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu"

Yeduthuni

Mmoja wa wanamuzi wakuu wa Daudi alikuwa na jina hili. Hii inaweza kumaanisha ni yeye.

Zaburi ya Daudi

Maana zinazowezekana ni 1) Daudi aliiandika zaburi au 2) zaburi inamhusu Daudi au 3) zaburi iko katika mtindo wa zaburi za Daudi.

wokovu wangu unatoka kwake

"yeye ndiye anayeniokoa"

Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu

Mwandishi anazungumzia uwezo wa mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni mwamba. "Yeye pekee ndiye anayeweza kunilinda na kuniokoa"

yeye ni mnara wangu wa juu

Mwandishi uwezo wa Mungu kumlinda kana kwamba Mungu ni mnara wa juu. "ananiepusha na kushikwa na adui"

sitasogezwa sana

"hakuna kitu kinachoweza kunisogeza kamwe"